Thursday, May 15, 2025
HUYU HAPA MWAMUZI MCHEZO WA FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO
Saturday, April 19, 2025
MRATIBU MISS TANZANIA AFARIKI DUNIA
Mratibu wa zamani wa Miss Tanzania Hashim Lundega, amefariki dunia leo Jijini Dar es Salaam.
Lundenga ambaye ameugua
kwa muda mrefu itakumbukwa ndio aliyesimamia kwa mafanikio makubwa Mashindano
ya Urembo Tanzania na kuyapa umaarufu mashindano hayo.
Lundenga pia aliwahi
kuhudumu kwenye Kamati ndani ya Klabu ya Yanga.
Thursday, April 17, 2025
SIMBA YALAMBA MKATABA MNONO
Mkataba Wa Simba Sports
Club Na JayRutty ni wa Shilingi Bilioni 38 kwa miaka mitano.
Kuna gawiwo la 5.6 Bilioni kila mwaka na ongezeko la asilimia 10 kwa kila mwaka
FAIDA ZA KIMKATABA.
1. Ujenzi wa Uwanja wa
Bunju (Watu Elf10 hadi 12).
2. Gari la IRIZAR .
3. Media production.
4. Ujenzi wa Ofisi Mpya
5. Kukuza Vipaji ( pesa
cash kutolewa)
6. Pre seasons
sponsorship
7. Medica room
8. Simba Day ( pesa
itatolewa cash m100)
9. Motisha kwa
wachezaji ( M470 cash)
10. Jezi za brand kubwa
dunia
YANGA TANGA,SIMBA MANYARA
SHIRIKISHO la Soka Tanzania(TFF) limepanga mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya CRDB Federation Cup kati ya bingwa mtetezi Yanga SC dhidi ya JKT Tanzania kufanyika katika dimba la CCM Mkwakwani Jijini Tanga.
Nusu fainali nyingine imepangwa kuchezwa katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa Manyara ikiwakutanisha Simba SC dhidi ya Singida Black Stars.
Michezo hiyo ya
kuwatafuta wanafainali wa Federation Cup 2024-2025 imepangwa kufanyika kati ya
Mei 16-18, 2025.
Tuesday, April 8, 2025
ARSENAL KUIVAA REAL MADRID USIKU WA LEO UEFA
Klabu ya Arsenal ya Uingereza, usiku wa leo inawakaribisha mabingwa mara 15 wa Ulaya, Real Madrid katika mechi ya kwanza ya hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA), katika mchezo utakaofanyika kwenye uwanja wa Emirates, jijini London.







