Klabu ya Arsenal ya Uingereza, usiku wa leo inawakaribisha mabingwa mara 15 wa Ulaya, Real Madrid katika mechi ya kwanza ya hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA), katika mchezo utakaofanyika kwenye uwanja wa Emirates, jijini London.
Timu hizo zilikutana kwa mara ya mwisho kwenye msimu wa UEFA 2005/06, ambapo ‘The Gunners’ ilisonga mbele kuelekea hatua ya robo fainali kwa ushindi wa wa 1-0 dhidi ya Real Madrid.

No comments:
Post a Comment