Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, October 27, 2014

KIJANA AKUTWA NA SHORTGUN NA RISASI 7 CHUMBANI KWAKE



POLISI mkoani Mbeya inamshikilia mkazi wa mtaa wa Pambogo maeneo ya Airport Jijini Mbeya kwa tuhuma za kukutwa na bunduki aina ya Short Gun na risasi saba alizokuwa akizimiliki kinyume cha sheria.

Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya Ahmed Msangi,amemtaja anayeshikiliwa kwa tuhuma hizo kuwa ni Emmanuel Mwakeja(27).

Kwa mujibu wa kamanda Msangi kijana Emmanuel amekamatwa Oktoba 26 mwaka huu majira ya saa 12:40 jioni akiwa nyumbani kwake Pambogo.

Kamanda Msangi alisema awali siku hiyo mnamo majira ya saa 11 jioni maeneo ya uwanja wa Sokoine katika kata ya Sisimba mkazi wa vMakunguru jijini hapa Alfonce Mwakasege(38) aligundua kuibiwa pikipiki yake aina ya Kinglion yenye namba za usajiri T 683 BDM.

Amesema baada ya kufanyika kwa msako wa haraka juu ya wizi wa pikipiki hiyo ndipo walikamatwa watuhumiwa wawili Joseph Kigulu(24) mkazi wa Airport na Juma Nelson(31) mkazi wa Iyela wote jijini Mbeya na walipohojiwa wakasema pikipiki hiyo ipo nyumbani kwa Emmanuel.

Kamanda Msangi amesema mara baada ya kwenda nyumbani kwa kijana huyo na kufanya upekuzi ndipo alipokutwa na bunduki aina ya Shortgun na risasi saba alizokuwa amezificha chini ya Godoro.

Amesema watuhumiwa wote wanashikiliwa na jeshi hilo na watafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika.

No comments:

Post a Comment