Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, April 12, 2026

DC NYAKIA ASISITIZA MICHEZO KWA AFYA NA UCHUMI

 




Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Wilaya ya Sumbawanga, Nyakia Ally Chirukile amesisitiza kuwa michezo ni muhimu katika kuimarisha Afya na Uchumi wa wananchi hivyo ni muhimu kila mwanajamii wakiwemo watumishi kuizingatia.

 

Chirukile ameyasema hayo wakati akifungua Bonanza la Michezo la watumishi lililofanyika katika Uwanja wa Kumbukumbu wa Nelson Mandela uliopo katika Manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa.

 

Chirukile amesema kuwa michezo sio tu hufungua fursa za kiuchumi, bali pia huimarisha undugu na mshikamano baina ya jamii.

 

"Michezo ni afya, michezo hufungua fursa za uchumi na kuimarisha undugu baina ya Jamii hivyo mabonanza kama haya yafanyike mara kwa mara ili kuchechemua maendeleo endelevu baina yetu," amesema Chirukile.

 

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amesisitiza kuwa Serikali inaunga mkono michezo katika jamii na kuwahamasisha wananchi kushiriki katika shughuli za michezo ili kuboresha afya zao na kuchangia maendeleo ya uchumi wa Taifa.

 

Bonanza hilo limehusisha timu kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Wilaya ya Mbozi na Wilaya ya Nkasi, zikishindana katika michezo mbalimbali kama vile mpira wa miguu, mpira wa pete, mpira wa mikono, mpira wa wavu, bao, drafti, na karata.

No comments:

Post a Comment