Lyamba Lya Mfipa
Na Joachim Nyambo
Thursday, May 15, 2025
HUYU HAPA MWAMUZI MCHEZO WA FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO
Saturday, April 19, 2025
MRATIBU MISS TANZANIA AFARIKI DUNIA
Mratibu wa zamani wa Miss Tanzania Hashim Lundega, amefariki dunia leo Jijini Dar es Salaam.
Lundenga ambaye ameugua
kwa muda mrefu itakumbukwa ndio aliyesimamia kwa mafanikio makubwa Mashindano
ya Urembo Tanzania na kuyapa umaarufu mashindano hayo.
Lundenga pia aliwahi
kuhudumu kwenye Kamati ndani ya Klabu ya Yanga.
Thursday, April 17, 2025
SIMBA YALAMBA MKATABA MNONO
Mkataba Wa Simba Sports
Club Na JayRutty ni wa Shilingi Bilioni 38 kwa miaka mitano.
Kuna gawiwo la 5.6 Bilioni kila mwaka na ongezeko la asilimia 10 kwa kila mwaka
FAIDA ZA KIMKATABA.
1. Ujenzi wa Uwanja wa
Bunju (Watu Elf10 hadi 12).
2. Gari la IRIZAR .
3. Media production.
4. Ujenzi wa Ofisi Mpya
5. Kukuza Vipaji ( pesa
cash kutolewa)
6. Pre seasons
sponsorship
7. Medica room
8. Simba Day ( pesa
itatolewa cash m100)
9. Motisha kwa
wachezaji ( M470 cash)
10. Jezi za brand kubwa
dunia
YANGA TANGA,SIMBA MANYARA
SHIRIKISHO la Soka Tanzania(TFF) limepanga mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya CRDB Federation Cup kati ya bingwa mtetezi Yanga SC dhidi ya JKT Tanzania kufanyika katika dimba la CCM Mkwakwani Jijini Tanga.
Nusu fainali nyingine imepangwa kuchezwa katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa Manyara ikiwakutanisha Simba SC dhidi ya Singida Black Stars.
Michezo hiyo ya
kuwatafuta wanafainali wa Federation Cup 2024-2025 imepangwa kufanyika kati ya
Mei 16-18, 2025.
Tuesday, April 8, 2025
ARSENAL KUIVAA REAL MADRID USIKU WA LEO UEFA
Klabu ya Arsenal ya Uingereza, usiku wa leo inawakaribisha mabingwa mara 15 wa Ulaya, Real Madrid katika mechi ya kwanza ya hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA), katika mchezo utakaofanyika kwenye uwanja wa Emirates, jijini London.
Tuesday, January 28, 2025
Wednesday, November 20, 2024
Saturday, November 16, 2024
TYSON AAMBULIA KICHAPO
Jake Paul amemshinda bondia nguli Mike Tyson kupitia uamuzi wa Pamoja katika mpambano wa uzito wa juu uliofanyika Texas Marekani. Pigano kati ya Paul, mtengeneza maudhui mwenye umri wa miaka 27 na Tyson, bingwa wa zamani wa uzito wa juu mwenye umri wa miaka 58, halikuwaridhisha mashabiki.
Mkongwe Tyson hakuweza kuonesha makali dhidi ya mpinzani wake huyo chipukizi. Tyson alimrushia ngumi 18 tu wakati Paul akimnyeshea nvua ya ngumi 78. Pigano hilo lilienda raundi zote nane. Jaji mmoja alimpa Paul pointi 80 dhidi ya 72 wakati wengine wawili wakimpa pointi 79-73.
Friday, November 15, 2024
KAMANDA KUZAGA ATOA SOMO KWA WANAVYUO MBEYA AKIFUNGUA DREAMS INTERCOLLEGE
Na Mwandishi Wetu
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga amewataka wanavyuo mkoani Mbeya kujiepusha na vitendo visivyofaa katika jamii ikiwemo uhalifu.
YANGA YAACHANA RASMI NA GAMOND
Uongozi wa klabu ya Yanga Sc umethibitisha kuvunja mkataba na kocha wa kikosi cha kwanza Miguel Angel Gamondi raia wa Argentina pamoja na kocha msaidizi Moussa Ndaw.

















