Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, May 15, 2025

HUYU HAPA MWAMUZI MCHEZO WA FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO


 Baada ya kuthibitishwa kwa uwanja wa mechi, Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) limetangaza uteuzi rasmi wa waamuzi kwa fainali ya Kombe la Shirikisho la CAF.

CAF imemteua mwamuzi wa kimataifa kutoka Mauritania, Dahane Beida, kuwa mwamuzi wa kati katika mchezo wa marudiano wa fainali ya Kombe la Shirikisho la CAF kati ya Simba SC ya Tanzania na RS Berkane ya Morocco. Mchezo huo umepangwa kufanyika tarehe 25 Mei 2025 katika Uwanja wa Amaan Zanzibar.
Dahane Beida ni mwamuzi mwenye uzoefu mkubwa katika soka la Afrika. Miongoni mwa mechi kubwa alizowahi kuzisimamia ni fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2023 kati ya Ivory Coast na Nigeria. Pia, alisimamia mechi ya marudiano ya fainali ya Kombe la Shirikisho la CAF msimu wa 2022/23.
Fainali ya mwaka huu inatarajiwa kuwa ya kusisimua, kwani Simba SC itakuwa inacheza fainali yake ya kwanza ya Kombe la Shirikisho, huku RS Berkane wakitafuta taji lao la tatu katika mashindano haya, baada ya kulibeba mwaka 2020 na 2022.
Mchezo wa kwanza wa fainali hiyo utafanyika tarehe 17 Mei 2025 katika Uwanja wa Berkane Municipal, Morocco.

Saturday, April 19, 2025

MRATIBU MISS TANZANIA AFARIKI DUNIA

 


Mratibu wa zamani wa Miss Tanzania Hashim Lundega, amefariki dunia leo Jijini Dar es Salaam.

Lundenga ambaye ameugua kwa muda mrefu itakumbukwa ndio aliyesimamia kwa mafanikio makubwa Mashindano ya Urembo Tanzania na kuyapa umaarufu mashindano hayo.

Lundenga pia aliwahi kuhudumu kwenye Kamati ndani ya Klabu ya Yanga.

Thursday, April 17, 2025

SIMBA YALAMBA MKATABA MNONO

 


Mkataba Wa Simba Sports Club Na JayRutty ni wa Shilingi Bilioni 38 kwa miaka mitano.

Kuna gawiwo la 5.6 Bilioni kila mwaka na ongezeko la asilimia 10 kwa kila mwaka 

FAIDA ZA KIMKATABA.

1. Ujenzi wa Uwanja wa Bunju (Watu Elf10 hadi 12).

2. Gari la IRIZAR .

3. Media production.

4. Ujenzi wa Ofisi Mpya

5. Kukuza Vipaji ( pesa cash kutolewa)

6. Pre seasons sponsorship

7. Medica room

8. Simba Day ( pesa itatolewa cash m100)

9. Motisha kwa wachezaji ( M470 cash)

10. Jezi za brand kubwa dunia

YANGA TANGA,SIMBA MANYARA



SHIRIKISHO la Soka Tanzania(TFF) limepanga mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya CRDB Federation Cup kati ya bingwa mtetezi Yanga SC dhidi ya JKT Tanzania kufanyika katika dimba la CCM Mkwakwani Jijini Tanga.

Nusu fainali nyingine imepangwa kuchezwa katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa Manyara ikiwakutanisha Simba SC dhidi ya Singida Black Stars. 

Michezo hiyo ya kuwatafuta wanafainali wa Federation Cup 2024-2025 imepangwa kufanyika kati ya Mei 16-18, 2025.

Tuesday, April 8, 2025

ARSENAL KUIVAA REAL MADRID USIKU WA LEO UEFA

 

Klabu ya Arsenal ya Uingereza, usiku wa leo inawakaribisha mabingwa mara 15 wa Ulaya, Real Madrid katika mechi ya kwanza ya hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA), katika mchezo utakaofanyika kwenye uwanja wa Emirates, jijini London.

Timu hizo zilikutana kwa mara ya mwisho kwenye msimu wa UEFA 2005/06, ambapo ‘The Gunners’ ilisonga mbele kuelekea hatua ya robo fainali kwa ushindi wa wa 1-0 dhidi ya Real Madrid.
Je, Arsenal itafanya maajabu leo mbele ya mabingwa hao wa kihistoria wa Ulaya?

Saturday, November 16, 2024

TYSON AAMBULIA KICHAPO


Jake Paul amemshinda bondia nguli Mike Tyson kupitia uamuzi wa Pamoja katika mpambano wa uzito wa juu uliofanyika Texas Marekani. Pigano kati ya Paul, mtengeneza maudhui mwenye umri wa miaka 27 na Tyson, bingwa wa zamani wa uzito wa juu mwenye umri wa miaka 58, halikuwaridhisha mashabiki.

Mkongwe Tyson hakuweza kuonesha makali dhidi ya mpinzani wake huyo chipukizi. Tyson alimrushia ngumi 18 tu wakati Paul akimnyeshea nvua ya ngumi 78. Pigano hilo lilienda raundi zote nane. Jaji mmoja alimpa Paul pointi 80 dhidi ya 72 wakati wengine wawili wakimpa pointi 79-73.

"Kwanza kabisa, Mike Tyson – ni heshima kupambana naye ulingoni," alisema Paul. Mike, yeye ni mkongwe, nimetiwa moyo naye, na tusingekuwa hapa leo bila yeye.”

Naye Tyson baada ya kichapo alisema, “Nilijua ni bondia mzuri. Alikuwa amejiandaa. Nilikuja kupigana. Sikumdhihirishia yeyote kitu, ila mimi mwenyewe.”

Kwa hisani ya DW

ANASEMA KOCHA MPYA WA YANGA

 


Friday, November 15, 2024

KAMANDA KUZAGA ATOA SOMO KWA WANAVYUO MBEYA AKIFUNGUA DREAMS INTERCOLLEGE



Na Mwandishi Wetu

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga amewataka wanavyuo mkoani Mbeya kujiepusha na vitendo visivyofaa katika jamii ikiwemo uhalifu.

Hayo ameyasema Novemba 14, 2024 wakati akifungua mashindano ya mpira wa miguu yanayohusisha vyuo vikuu mkoani humo yanayojulikana kama "Dreams Intercollege" yaliyofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge Jijini Mbeya.
Kamanda Kuzaga amewataka wanavyuo mkoani humo kuyatumia mashindano hayo kama sehemu ya kujenga upendo, umoja, mshikamano na kufahamiana kati ya chuo na chuo na wanavyuo na sio uadui.
Aliongeza kuwa, mashindano hayo yakawe chachu katika kuibua vipaji vya mpira wa miguu kwa wanavyuo mkoani humo kwani michezo ni ajira hivyo alisisitiza kutumia vizuri fursa ya kuanzishwa kwa mashindano hayo.
Naye, Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Mbeya Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Veronica Ponera amewataka wanavyuo mkoani humo kujiepusha na ukatili wa kijinsia, kujiepusha na tamaa ya vitu vya thamani ambavyo vinaweza kuwaingiza kwenye vishawishi vya vitendo viovu.
"Jeshi la Polisi nchini linaendelea na kampeni ya Tuwaambie kabla hawajaharibiwa hivyo ni nafasi kwetu kuwaeleza wanavyuo mambo ya kujiepusha nayo kabla hamjaharibikiwa na kupoteza dira ya kufikia ndoto zenu" alisema ASP Ponera.
Awali akizungumza Mratibu wa mashindano hayo Meneja wa kituo cha redio"Dreams fm" cha Jijini Mbeya ndugu Samuel Mhina amesema kuwa mashindano hayo yatashirikisha wanavyuo wote waliopo mkoani Mbeya, T.I.A ambaye ni bingwa mtetezi, CUoM, Tumaini, MUST, Chuo cha Afya - Ifisi yakiwa na lengo la kujenga umoja na kuibua vipaji.
Mechi ya ufunguzi ambayo iliwakutanisha chuo kikuu cha katoliki Mbeya (CUoM) dhidi ya T.I.A imemalizika kwa kushuhudia CUoM ikiibuka na ushindi wa magoli matano kwa bila na kukabidhiwa ngao ya jamii ikiwa ni ishara ya ufunguzi wa mashindano hayo.

YANGA YAACHANA RASMI NA GAMOND


Uongozi wa klabu ya Yanga Sc umethibitisha kuvunja mkataba na kocha wa kikosi cha kwanza Miguel Angel Gamondi raia wa Argentina pamoja na kocha msaidizi Moussa Ndaw.

Taarifa ya leo Novemba 15, 2024 iliyotolewa na klabu hiyo imebainisha kuwa klabu hiyo tayari imeanza mchakato wa haraka wa kutafuta Makocha wapya wa kikosi hicho na unatarajiwa kukamilika hivi punde.
“Uongozi wa Young Africans Sports Club unapenda kuwashukuru Makocha hao kwa mchango wao ndani ya Klabu yetu na unawatakia kila la kheri katika majukumu yao mapya.” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Thursday, November 14, 2024

KING KIKII AFARIKI DUNIA

Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi nchini Tanzania, Boniface Kikumbi maarufu King Kikii amefariki dunia.

Mwanamuziki huyo ambaye ameugua kwa muda mrefu, amefariki usiku wa kuamkia leo Novemba 15 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,Jijini Dar es Salaam ambako alikuwa akipatiwa matibabu

Marehemu King Kikii atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika muziki wa dansi Tanzania. Kwa miaka mingi ameburudisha, amefundisha na kuelimisha jamii kupitia nyimbo zake.

Enzi za uhai wake,Marehemu King Kikiii alitamba na vibao mbalimbali kikiwemo cha 'Kitambaa cheupe'.

King Kikii alikuwa Mtunzi na mwimbaji wa zamani wa Marquiz du Zaire na Orchestra Double O ambaye pia alikuwa mmiliki wa bendi ya La Capital, inayotesa na mtindo wake wa Kitambaa Cheupe

Alizaliwa mwaka 1947 katika Jiji la Lubumbashi lililopo kwenye Mkoa wa Katanga, eneo maarufu huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC)