Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, May 22, 2026

MADIWANI MBARALI WALIVYOTEMBELEA MRADI WA UJENZI WA UWANJA WA KISASA ARUSHA








Na Mwandishi Wetu

Ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kujifunza na kupata uzoefu kwenye masuala mbalimbali Jijini Arusha kati ya Mei 14 - 18, 2026, Wajumbe wa Baraza la Madiwani wakiwa wameambatana na Timu ya Wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, wametembelea na kujionea uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika ujenzi wa uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu unaojengwa Jijini humo.


Akizungumza baada ya kuhitimisha ziara hiyo, Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali ambaye ameongoza ujumbe huo, Charles Komba ameipongeza Serikali kwa uwekezaji huo ambao unaonesha dhamira ya dhati katika kuinua sifa ya nchi ya Tanzania kupitia sekta ya michezo ambapo kukamilika kwa uwanja huo ni uthibitisho kwa nchi yetu kuwa tayari kwa michuano ya AFCON 2027 na michuano mingine yenye hadhi kitaifa na kimataifa.


“Wanambarali tunampongeza Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhamasisha michezo kwa vitendo, uwanja huu ni uthibitisho kuwa Tanzania tuko tayari kwa AFCON 2027, na sisi Mbarali tunamuunga mkono kwa kuwa tumetambua fursa za uwekezaji kupitia mradi huu na tuko tayari kuzitumia”, amesema Komba.

Saturday, May 16, 2026

ACHIMWENE SAFARI YAAHIDI MAKUBWA TULIA TRUST MARATHON

 

Mwakilishi wa Kampuni ya Achimwene Safaris,Emmanuel Mwalupindi akitoa salamu za Kampuni kwenye kilele cha mashindano


Mwakilishi wa Kampuni ya Achimwene Safaris,Emmanuel Mwalupindi akipokea cheti cha utambuzi wa mchango wa kampuni hiyo katika mashindano ya mwaka huu kutoka kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust,Dk Tulia Ackson 



Mwakilishi wa Kampuni ya Achimwene Safaris akikabidhi zawadi kwa baadhi ya washindi wa mbio ndefu za fupi

Na Joachim Nyambo,Mbeya 

KAMPUNI ya Achimwenye Safaris imeahidi kuendelea kuyaunga mkono Mashindano ya Mbio ya Tulia Marathon ikisema inavutiwa na umuhimu wake ndani ya jamii hususani kwa kutumia kukusanya fedha kwaajili ya kuimarisha huduma za kijamii.

 

Miongoni mwa mambo yanayotajwa kuivutia Kampuni ya Achimwene Safari ni pamoja na fedha zinazokusanywa kupitia Tulia Marathon kutumika kuimarisha miundombinu hususani majengo ya sekta za Elimu na Afya na pia kuboresha maisha ya kaya zenye uhitaji.

 

Mwakilishi wa kampuni hiyo, Emmanuel Mwalupindi amebainisha hayo alipotoa salamu za kampuni kwenye kilele cha Mashindano ya Mbio za Betika Mbeya Tulia Marathon 2026 yaliyofanyika jijini Mbeya ikiwa ni msimu wa 10 huku Achimwene Safari ikiwa ni miongoni mwa wadau waliofadhili.

 

“Tunaridhishwa kwa namna mashindano yanavyofanyika,ni faraja kuona fedha zinazokusanywa zinakwenda kuisaidia jamii iliyo na uhitaji.Sisi Achimwene Safari tunakuahid Mkurugenzi kuwa tutazidi kuwa nawe bega kwa bega..hatutokuacha.” amesema Mwalupindi.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust iliyoandaa mashindano hayo,Dk Tulia Ackson ameipongeza kampuni ya Achimwene Safaris kwa kuunga mkono juhudi za taasisi hiyo kwa kuwa sehemu ya wadhamini ili kufikia adhma ya kuwafikia wenye uhitaji.

 

Dk Tulia ambaye pia ni Mbunge wa Uyole,Spika wa Bunge mstaafu na Rais wa Mabunge Duniani(IPU) amewataka wadau wengine wakiwemo wa usafiri kuiga mfano wa Achimwene Safaris kushiriki kwa kufadhili mashindano hayo kwakuwa pamoja na faida nyingine pia yanafunguwa fursa katika nyanja ya usafirishaji kutokana na wageni wanaofika mkoani Mbeya kushiriki.

 

Mashindano ya Betika Mbeya Tulia Marathon  mwaka huu pia yamehudhuliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo,Gerson Msigwa aliyemwakilisha Waziri wa Wizara hiyo,Paul Makonda huku pia  wasanii mbalimbali maarufu wa tasnia ya uigizaji na wao wakishiriki mbio hizo.


Friday, May 15, 2026

UWANJA WA YANGA KUMILIKIWA NA KAMPUNI

 




RAIS wa Klabu ya Yanga Eng.Hers Said amesema Klabu ya Yanga itafungua kampuni itakayohusika na umiliki wa Uwanja utakaojengwa ili kuepusha migongano ya kimaslahi baina ya wamiliki wa timu na wa uwanja.

 

“Hii itakuwa ni speho project na lazima iwe na uongozi wake,iwe na umiliki wake.Klabu inataka kujenga uwanja na mwekezaji ameshapatikana.Hivyo klabu ya Yanga kwa kushirikiana na mwekezaji wetu tutafungua kampuni.”

 

“Kampuni hiyo ndiyo itakayomiliki uwanja na katika kampuni hiyo itakayomiliki uwanja asilimia hamsini itakwenda kwa Young Africans na asilimia 50 itakwenda kwa mwekezaji.”

 

“GSM amekubali kumiliki uwanja kwa asilimia 50/50 na Yanga. GSM hana tamaa, angekuwa na tamaa basi angesema anataka asilimia 80. Tunajua wapo wenye tamaa na tunawajua. Ukiacha msemo wa Yanga Bingwa, hatimaye GSM ametupatia msemo mwingine, kuanzia sasa Msemo wetu ni “GSM HANA TAMAA” Eng. Hersi

 

Amesema mchango wa Yanga kwenye mradi huo wa uwekezaji mpya ni kutoa ardhi yake inayojengwa uwanja.


MBEYA TULIA MARATHON 2026 NI KIVUMBI NA JASHO

 









WATOTO WALIVYOINOGESHA BETIKA MBEYA TULIA MARATHON 2026 SIKU YA KWANZA

 














Thursday, May 14, 2026

MWASITI NA BARBARA WAKABIDHI TAULO ZA KIKE SHULE YA SEKONDARI IDUDA












Na Mwandishi Wetu

KUELEKEA mbio za Betika Mbeya Tulia Marathon 2026 Mabalozi wa Tulia Trust, Mwasiti Almas Yusuph maarufu kama Mwasiti na Barbara Hassan wamefika katika shule ya sekondari Iduda iliyopo katika Kata ya Iduda Jimbo la Uyole Jijini Mbeya.

 

Mabalozi hawa wamefika shuleni hapo kwa lengo kuu la kufanya mdahalo na wanafunzi wa shule wenye mada isemayo “Maisha kabla ya umaarufu na safari ya mafanikio” huku pia wakigawa taulo za kike.

 

Mdahalo huu umefanyika kupitia simulizi za wageni maarufu ambapo ikiaminiwa kuwa wanafunzi watajifunza kuwa mafanikio hayaji kwa bahati, bali hujengwa kwa nidhamu, kujituma na kutokukata tamaa.