Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, May 16, 2026

ACHIMWENE SAFARI YAAHIDI MAKUBWA TULIA TRUST MARATHON

 

Mwakilishi wa Kampuni ya Achimwene Safaris,Emmanuel Mwalupindi akitoa salamu za Kampuni kwenye kilele cha mashindano


Mwakilishi wa Kampuni ya Achimwene Safaris,Emmanuel Mwalupindi akipokea cheti cha utambuzi wa mchango wa kampuni hiyo katika mashindano ya mwaka huu kutoka kwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust,Dk Tulia Ackson 



Mwakilishi wa Kampuni ya Achimwene Safaris akikabidhi zawadi kwa baadhi ya washindi wa mbio ndefu za fupi

Na Joachim Nyambo,Mbeya 

KAMPUNI ya Achimwenye Safaris imeahidi kuendelea kuyaunga mkono Mashindano ya Mbio ya Tulia Marathon ikisema inavutiwa na umuhimu wake ndani ya jamii hususani kwa kutumia kukusanya fedha kwaajili ya kuimarisha huduma za kijamii.

 

Miongoni mwa mambo yanayotajwa kuivutia Kampuni ya Achimwene Safari ni pamoja na fedha zinazokusanywa kupitia Tulia Marathon kutumika kuimarisha miundombinu hususani majengo ya sekta za Elimu na Afya na pia kuboresha maisha ya kaya zenye uhitaji.

 

Mwakilishi wa kampuni hiyo, Emmanuel Mwalupindi amebainisha hayo alipotoa salamu za kampuni kwenye kilele cha Mashindano ya Mbio za Betika Mbeya Tulia Marathon 2026 yaliyofanyika jijini Mbeya ikiwa ni msimu wa 10 huku Achimwene Safari ikiwa ni miongoni mwa wadau waliofadhili.

 

“Tunaridhishwa kwa namna mashindano yanavyofanyika,ni faraja kuona fedha zinazokusanywa zinakwenda kuisaidia jamii iliyo na uhitaji.Sisi Achimwene Safari tunakuahid Mkurugenzi kuwa tutazidi kuwa nawe bega kwa bega..hatutokuacha.” amesema Mwalupindi.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust iliyoandaa mashindano hayo,Dk Tulia Ackson ameipongeza kampuni ya Achimwene Safaris kwa kuunga mkono juhudi za taasisi hiyo kwa kuwa sehemu ya wadhamini ili kufikia adhma ya kuwafikia wenye uhitaji.

 

Dk Tulia ambaye pia ni Mbunge wa Uyole,Spika wa Bunge mstaafu na Rais wa Mabunge Duniani(IPU) amewataka wadau wengine wakiwemo wa usafiri kuiga mfano wa Achimwene Safaris kushiriki kwa kufadhili mashindano hayo kwakuwa pamoja na faida nyingine pia yanafunguwa fursa katika nyanja ya usafirishaji kutokana na wageni wanaofika mkoani Mbeya kushiriki.

 

Mashindano ya Betika Mbeya Tulia Marathon  mwaka huu pia yamehudhuliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo,Gerson Msigwa aliyemwakilisha Waziri wa Wizara hiyo,Paul Makonda huku pia  wasanii mbalimbali maarufu wa tasnia ya uigizaji na wao wakishiriki mbio hizo.


No comments:

Post a Comment