Na Mwandishi Wetu
Ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kujifunza na kupata uzoefu kwenye masuala mbalimbali Jijini Arusha kati ya Mei 14 - 18, 2026, Wajumbe wa Baraza la Madiwani wakiwa wameambatana na Timu ya Wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, wametembelea na kujionea uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika ujenzi wa uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu unaojengwa Jijini humo.
Akizungumza baada ya kuhitimisha ziara hiyo, Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali ambaye ameongoza ujumbe huo, Charles Komba ameipongeza Serikali kwa uwekezaji huo ambao unaonesha dhamira ya dhati katika kuinua sifa ya nchi ya Tanzania kupitia sekta ya michezo ambapo kukamilika kwa uwanja huo ni uthibitisho kwa nchi yetu kuwa tayari kwa michuano ya AFCON 2027 na michuano mingine yenye hadhi kitaifa na kimataifa.







No comments:
Post a Comment