Na Mwandishi Wetu
KUELEKEA mbio za Betika
Mbeya Tulia Marathon 2026 Mabalozi wa Tulia Trust, Mwasiti Almas Yusuph maarufu
kama Mwasiti na Barbara Hassan wamefika katika shule ya sekondari Iduda iliyopo
katika Kata ya Iduda Jimbo la Uyole Jijini Mbeya.
Mabalozi hawa wamefika
shuleni hapo kwa lengo kuu la kufanya mdahalo na wanafunzi wa shule wenye mada
isemayo “Maisha kabla ya umaarufu na safari ya mafanikio” huku pia wakigawa
taulo za kike.
Mdahalo huu umefanyika
kupitia simulizi za wageni maarufu ambapo ikiaminiwa kuwa wanafunzi watajifunza
kuwa mafanikio hayaji kwa bahati, bali hujengwa kwa nidhamu, kujituma na
kutokukata tamaa.











No comments:
Post a Comment