RAIS wa Klabu ya Yanga
Eng.Hers Said amesema Klabu ya Yanga itafungua kampuni itakayohusika na umiliki
wa Uwanja utakaojengwa ili kuepusha migongano ya kimaslahi baina ya wamiliki wa
timu na wa uwanja.
“Hii itakuwa ni speho
project na lazima iwe na uongozi wake,iwe na umiliki wake.Klabu inataka kujenga
uwanja na mwekezaji ameshapatikana.Hivyo klabu ya Yanga kwa kushirikiana na
mwekezaji wetu tutafungua kampuni.”
“Kampuni hiyo ndiyo
itakayomiliki uwanja na katika kampuni hiyo itakayomiliki uwanja asilimia
hamsini itakwenda kwa Young Africans na asilimia 50 itakwenda kwa mwekezaji.”
“GSM amekubali kumiliki
uwanja kwa asilimia 50/50 na Yanga. GSM hana tamaa, angekuwa na tamaa basi
angesema anataka asilimia 80. Tunajua wapo wenye tamaa na tunawajua. Ukiacha
msemo wa Yanga Bingwa, hatimaye GSM ametupatia msemo mwingine, kuanzia sasa
Msemo wetu ni “GSM HANA TAMAA” Eng. Hersi
Amesema mchango wa
Yanga kwenye mradi huo wa uwekezaji mpya ni kutoa ardhi yake inayojengwa
uwanja.




No comments:
Post a Comment