Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, May 15, 2026

UWANJA WA YANGA KUMILIKIWA NA KAMPUNI

 




RAIS wa Klabu ya Yanga Eng.Hers Said amesema Klabu ya Yanga itafungua kampuni itakayohusika na umiliki wa Uwanja utakaojengwa ili kuepusha migongano ya kimaslahi baina ya wamiliki wa timu na wa uwanja.

 

“Hii itakuwa ni speho project na lazima iwe na uongozi wake,iwe na umiliki wake.Klabu inataka kujenga uwanja na mwekezaji ameshapatikana.Hivyo klabu ya Yanga kwa kushirikiana na mwekezaji wetu tutafungua kampuni.”

 

“Kampuni hiyo ndiyo itakayomiliki uwanja na katika kampuni hiyo itakayomiliki uwanja asilimia hamsini itakwenda kwa Young Africans na asilimia 50 itakwenda kwa mwekezaji.”

 

“GSM amekubali kumiliki uwanja kwa asilimia 50/50 na Yanga. GSM hana tamaa, angekuwa na tamaa basi angesema anataka asilimia 80. Tunajua wapo wenye tamaa na tunawajua. Ukiacha msemo wa Yanga Bingwa, hatimaye GSM ametupatia msemo mwingine, kuanzia sasa Msemo wetu ni “GSM HANA TAMAA” Eng. Hersi

 

Amesema mchango wa Yanga kwenye mradi huo wa uwekezaji mpya ni kutoa ardhi yake inayojengwa uwanja.


No comments:

Post a Comment