Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, February 27, 2015

WANAHABARI WANAHARAKATI WA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA WANENA

 Mhariri mkuu wa blogu ya Lyamba Lya Mfipa Bw.Joachim Nyambo(Wa tatu kulia) akifuatilia jambo kwa makina wakati darasa likiendelea.
 Mmoja wa wanahabari washiriki wa mafunzo akichangia hoja.
Mwahabari mkongwe nchini Wence Mushi(Mbele) akiendelea kufundisha wana warsha katika hoteli ya Ruaha mjini Iringa.
 Kutoka kulia ni wanahabari kutoka Mbeya Thompson Mpanji,Esther Macha na mhariri mkuu wa Lyamba Lya Mfipa wakifuatilia mafunzo yanayotolewa na Bw.Mushi.

                      HABARI KAMILI TOKA IRINGA

KUTOPEWA kipaumbele kwa ofisi za maafisa jamii na maendeleo katika bajeti kumetajwa kuwa miongoni mwa mambo yanayochangia kwa kiasi kikubwa vitendo vya ukatili wa kijinsia kuendelea kushamiri katika jamii.

Hayo yamebainishwa na wanahabari walioko kwenye mafunzo ya masuala ya ukatili wa kijinsia yanayofanyika mkoani Iringa yakiwa yameandaliwa na Chama cha waandishi wa habari wanawake(Tamwa) ambapo washiriki wanatoka katika mikoa ya Mbeya,Iringa,Njombe na Ruvuma.

Wanahabari hao wamesema ofisi za maafisa ustawi wa jamii zinakabiliwa na changamoto ya uhaba wa fedha kutokana na halmashauri nyingi kutozipa kipaumbele ofisi hizo wakati wa upangaji wa bajeti.

Mmoja wa wanahabari hao Geofray Nihahi amesema wengi wa maofisda kutoa ofisi hizo wamekuwa wakilalamika kukosa fedha na ndiyo sababu hawatekelezi majukumu yao ipasavyo na badala yake wamebakia maofisini ambako kimsingi hawana kazi zaidi ya kupiga soga.

Nihahi amesema uhaba huo wa fedha umesababisha maafisa hao kushinda kutekeleza majukumu waliyopewa ikiwemo utoaji elimu kwa jamii juu ya madhara ya ukatili wa kijinsia hivyo kusababisha vitendo vya ukatili kuendelea kukithiri.

Naye Cresensia Kapinga amesema ni wakati kwa wadau wa masuala ya kijamii kujiuliza kwa kila mmoja ni kwa namna gani ameweza kujitoa katika kuhakikisha anakomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye jamii inayomzunguka na iwapo hajafanya basi atambue kuwa ana deni la kutekeleza hayo.

Kwa upande wake Tumaini Msowoya,amesema bado katika jamii kuna matukio mengi ya ukatili wa kijinsia na pia ukatili dhidi ya watoto ambao baadhi ya wanajamii wanaufanya pasipo kujua kuwa wanakosea.

No comments:

Post a Comment