Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, April 25, 2026

Uzinduzi Pre-Betika Mbeya Tulia Marathon 2026 wafana

 





Na Mwandishi Wetu

 

KATIBU Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Mohamed Azizi leo amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Beno Malisa kufungua Tamasha la Pre-Betika Mbeya Tulia Marathon 2026 lililofanyika ndani ya Dimba la Sokoine

 

Kufanyika kwa Tamasha hilo ni sehemu ya maandalizi ya kuelekea mashindano ya riadha ya Betika Mbeya Tulia Marathon yatakayofanyika Mei 15-16 Mwaka huu ndani ya uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya kwa lengo la kukusanya fedha kwaajili ya kusaidia jamii.

 

Azizi amesema anatamani kuona mwaka huu mashindano hayo ya riadha yanashirikisha washiriki wengi zaidi kutoka ndani na nje ya nchi na kuwataka wakazi jijini Mbeya hasa vijana kuchangamkia fursa ya ujio wa wageni kufanya shughuli za kiuchumi.

 

“Wageni wengi watakuja sasa ni wakati wa vijana kuchangamka,watakaouza vyakul,vinywaji,bodaboda watasafirisha watu na nyumba za kulala wageni pia zitafanya biashara.”


Uzinduzi wa Pre-Betika Mbeya Tulia Marathon 2026 awali ulitanguliwa na mbio za pole(Joging) zilizoanzia eneo la Kituo kidogo cha mabasi cha Kabwe hadi Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya zikishirikisha vikundi mbalimbali vya mbio hizo.

No comments:

Post a Comment