Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, June 13, 2026

ATUPWA JELA MIAKA 30 KWA KULAWITI

 


Na Mwandishi Wetu,Kyela

MAHAKAMA ya Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya imemuhukumu Agen Mwakyusa (34) Mkazi wa Kijiji cha Busoka Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kulawiti alilolitenda kwa mama mwenye umri wa miaka 49 baada ya kumvamia akiwa amelala nyumbani kwake kisha kumwingilia kwa nguvu kinyume na maumbile.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa mahakama hiyo Paul Barnabas Juni 12, 2026 ambapo aAkisoma hukumu hiyo,Hakimu Barnabas alisema kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Januari 02, 2026 baada ya kufika nyumbani kwa mhanga ambaye anaishi peke yake majira ya usiku wa manane kisha kuvunja mlango na kuingia ndani na kutekeleza adhima yake ya kihalifu.

Mwendesha mashitaka wa serikali Wakili Sharon Sekemi akiwa mahakamani hapo alimuomba Hakimu kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa huyo ili liwe fundisho kwake na vijana wengine wa kiume wenye tabia kama ya mshitakiwa. 

No comments:

Post a Comment