Na Mwandishi Wetu,Kyela
MAHAKAMA ya Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya imemuhukumu Agen Mwakyusa (34) Mkazi wa Kijiji cha Busoka Wilaya ya Kyela Mkoa wa Mbeya kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kulawiti alilolitenda kwa mama mwenye umri wa miaka 49 baada ya kumvamia akiwa amelala nyumbani kwake kisha kumwingilia kwa nguvu kinyume na maumbile.
Mwendesha mashitaka wa serikali Wakili Sharon Sekemi akiwa mahakamani hapo alimuomba Hakimu kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa huyo ili liwe fundisho kwake na vijana wengine wa kiume wenye tabia kama ya mshitakiwa.

No comments:
Post a Comment