Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, June 12, 2026

Barbara Hassan hapendi kusifia uwezo wake alipokuwa darasani

 

Aliyewahi kuwa mtangazaji wa Clouds FM,Couds TV na  Mjini FM,Barbara Hassan amewasihi wanafunzi kujenga tabia ya kusoma vitabu kwa lengo la kujijenga kujiamini huku wakiamini kuwa Ndani ya Ndoto Inawezekana.

 

Alitoa ujumbe huu wakati wa kufanyika kwa mdahalo Iduda High School iliyopo Kkata ya Iduda Jimbo la Uyole uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa elimu kutoka ndani ya mkoa wa Mbeya.

 

Mdahalo huo uliandaliwa na Taasisi ya Tulia Trust ulikiwa na mada isemayo “Maisha kabla ya umaarufu na safari ya mafanikio” huku kauli mbiu ikisema “Kutoka kuwa ndoto hadi uhalisia”* huku wanafunzi wakihimizwa Kujifunza, kujiamini na kujitegemea.


No comments:

Post a Comment