Sunday, July 28, 2024
ALICHOKIANDIKA MWANASHERIA WA YANGA
MILIONI 10 KUKARABATI UWANJA WA SOKOINE
Na Lyamba Lya Mfipa
SHILINGI milioni kumi zinatarajiwa kutumika kwaajili ya ukarabati wa Uwanja wa Kumbumbu ya Sokoine lengo likiwa ni kuuweka kweny hadhi stahiki ya kutumiwa kwa mashindano mbalimbali ikiwemo Ligi kuu ya Tanzania bara.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Mbeya, Langaeli Akyoo
alisema kuwa maboresho yanayofanyika ni pamoja na kupaka rangi kwenye
viti vya kukalia mashabiki, kufunga seng'enge mpya na kujenga vibanda vipya vya
benchi la ufundi.
Akyoo alisema ukarabati huo ni utekelezaji wa maelekezo ya barua waliyopokea kutoka Shirikisho la soka
Tanzania (TFF) ya kuwataka wamiliki hao kufanya maboresho kadhaa katika uwanja
huo ili kuendana na viwango vinavyohitajika.
"Tulipokea barua kutoka TFF ikitutaka, kufanya ukarabati na
maboresho kadhaa, ikiwemo kupaka rangi viti vinavyokaliwa na mashabiki, kufunga
seng'enge vizuri kuzunguka uwanja na kujenga upya vibanda vinavyokaliwa na
benchi la ufundi, na tayari zoezi hili tunaendelea nalo" alisema Akyoo
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya, Patrick Mwalunenge, akiwa
ameongozana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (M-NEC), Ndele Jailos
Mwaselela na Katibu Mwenezi Christopher Uhagile jana walifika uwanjani hapo
kukagua maendeleo ya ukarabati huo unaoendelea.
Akiwa eneo la tukio Mwalunenge alisema kuwa wametenga zaidi ya
shilingi milioni 10 ambazo zitatumika kupaka rangi kuzunguka uwanja, na kudai
kuwa mpango uliopo ni kufanya ukarabati mkubwa ikiwa ni pamoja na kujenga
majukwaa ya mashabiki ili wasilowe na mvua pia kujenga vibanda vya kisasa vya
kufanyia biashara kuzunguka uwanja.
"Mpango wetu ni kuufanya uwanja wetu uvutie zaidi, kwahiyo
tunaendelea kutafuta wadau mbalimbali watakao tuunga mkono ili tufanye
maboresho makubwa sana kwenye uwanja wetu huu,
tutajenga majukwaa kuzunguka uwanja hata kama mvua inanyesha mashabiki
wasilowe, pia tuna mpango wa kufunga taa ili mpira uchezwe hata nyakati za usiku"
alisema Mwalunenge
Kwaupande wake Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (M-NEC),
Ndele Mwaselela alimpongeza Mwenyekiti Mwalunenge kwa jitihada hizo, kwa madai kuwa kazi hizi za kujitolea
zinahitaji zaidi moyo wa kujitoa.
Meneja wa uwanja Modestus Mwaluka alisema rangi inayopakwa
uwanjani hapo ni ya kijani na njano na kueleza kuwa mkandarasi aliyepewa kazi
hiyo anatarajia kukamilisha kazi hiyo ndani ya siku saba.
Yanga SC vs Kaizer Chiefs Toyota Cup leo
LEO, wananchi Yanga SC watakuwa dimbani kucheza na Kaizer Chiefs ni katika Kombe la Toyota
Mechi hii itapigwa kuanzia saa 10:00 jioni na kuruka mbashara AzamSports1HD
Ni pira Nabi ama pira Gamondi lipi kuondoka na ushindi?
Thursday, July 25, 2024
YANGA YAPATA MTEREMKO
Sunday, July 21, 2024
AL HILAL RASMI MSHINDI WA TATU DARPORT KAGAME CUP 2024
Al Hilal rasmi amechukua nafasi ya Mshindi wa Tatu wa Michuano ya Darport Kagame Cup 2024 baada ya mikwaju ya penati 3-2. Hii ni baada ya dakika 90 za mchezo kumalizika kwa sare ya kufungana 1-1 katika uwanja wa KMC Stadium.
RASTA WA HANS POPPE AFURAHIA KUTUA MSIMBAZI
“Nimejisikia furaha kwa sababu nimekuja katika timbu ambayo
nilikuwa naiota, nimekuwa naiwaza siku zote kwa hiyo nimefurahi kukutana na
wenzangu. Wenzangu wamenipokea vizuri na nimejiandaa kwaajili ya kuipambania
timu yangu”
Ni maneno ya mchezaji 'kiungo fundi wa mpira' Awesu Ally Awesu akiwa
mazoezini kwa mara ya kwanza na kikosi cha wekundu wa msimbazi baada ya kutua nchini
Misri.
Hatiamaye ametimiza ndoto ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya
Usajili ya Miamba wa Soka Nchini na Afrika Simba SC marehemu Zacharia Hans
Poppe ya kumuona akikipiga kunako wekundu wa Msimbazi, Simba Sc.
Ni jicho la ziada la kutambua
vipaji la Hans Pope ndilo lililomuibua kwa mara ya kwanza Awesu Awesu. Aliwahi
kuitwa Rasta wa Hans Poppe kutokana na utambulisho wake mkubwa wa mtindo wa
nywele.
Ilikuwa kwenye nusu fainali ya FA kati ya Madini SC dhidi ya Simba SC katika dimba la Sheikh Amri
Abeid wa jijini Arusha uliopigwa mwaka 2017. Awesu Awesu akichezea Madini ya
Arusha katika pambano lile alikiwasha na kuisumbua sana safu ya kiungo ya
Simba.
Ndipo jicho la Zacharia Hans Poppe lilipomuona kijana mwenye
Rasta ambaye aliisumbua kweli kweli
Simba. Katika pambano hilo Simba walishinda kwa taabu 1-0.
Baada ya pambano lile Hans Poppe alipiga picha ya ukumbusho na
Uwesu Awesu na kuzungumza naye mambo machache na inawezekana kubwa kabisa ni
hapo baadaye atue Msimbazi
Ni baada ya miaka nane sasa Awesu Awesu ametua Msimbazi na yupo
kambini Misri akijiwinda kwa msimu ujao wa mashindano mbalimbalj ikiwemo Ligi
kuu ya NBC.
Akiwa Misri Awesu Awesu amekaririwa akieleza furaha yake ya
kutimia kwa ndoto yake ya kutua katika timu ya moyo wake.
Saturday, July 20, 2024
Augsburg 2 - 1 Yanga
BAADA ya mechi kati ya Yanga SC
Maxi Nzengeli ndiye aliyetoa pasi ya goli lililofungwa na Mshambuliaji Jean Baleke.
Ni Yanga na Augsburg saa 10 leo
Mabingwa wa Tanzania Bara wako Afrika kusini ambapo leo majira ya saa 10 jioni kwa saa za Tanzania watashuka uwanja wa Mbombela huko Mpumalanga kuikabili Augsburg Fc katika mchezo wa ufunguzi michuano ya Mpumalanga International Cup
Friday, July 19, 2024
ASILI YA WAPOGOLO
Thursday, July 18, 2024
Tuesday, July 16, 2024
LIGI KUU YA NBC 2024/25 KUANZA AGOSTI 16
Bodi ya ligi kuu Tanzania Bara TPLB imetangaza Agosti 16 kuwa tarehe rasmi ya kuanza kwa ligi kuu ya NBC 2024-2025
Sunday, July 14, 2024
UJUE USAJIRI WA SIMBA 2024/25
Wachezaji (18) walioondoka Simba SC 2024/25
Saturday, July 13, 2024
YANGA YATUMA SALAMU BURUNDI
SADIO KANOUTE AKUTANA TENA NA BENCHIKHA
MNEC NDELE MWASELELA AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO MBEYA DC
Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (MNEC) Ndele Mwaselela amekabidhi vifaa vya michezo kwa timu 16 bora zinazoshiriki ligi ya Mama Samia Mshikamano Cup inayoendelea katika viunga vya wilaya hiyo, vifaa hivyo ni pamoja na mipira na jezi.Mwaselela amekabidhi vifaa hivyo vya michezo kwa timu 16 Julai 11, 2024 katika ofisi za CCM mkoa wa Mbeya.

































