Mabingwa wa ligi kuu nchini Burundi Vital'o wanatarajiwa kutumia uwanja wa Azam Complex katika mchezo wa mkondo wa kwanza hatua ya awali ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Yanga
Ni wazi sasa Yanga haitasafiri nje ya Tanzania katika mechi zake za hatua ya awali zitakazopigwa August 16-18 na August 24-26
Yanga inatarajiwa kutumia uwanja wa Benjamin Mkapa katika mechi ya mkondo wa pili
Msimu huu Yanga imeweka malengo makubwa katika michuano ya ligi ya mabingwa ambapo Wananchi wanautaka ubingwa wa Afrika

No comments:
Post a Comment