Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, July 25, 2024

YANGA YAPATA MTEREMKO

 


Mabingwa wa ligi kuu nchini Burundi Vital'o wanatarajiwa kutumia uwanja wa Azam Complex katika mchezo wa mkondo wa kwanza hatua ya awali ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Yanga

Vital'o wamelazimika kuleta mchezo huo Dar kwakuwa Burundi haina uwanja uliokidhi matakwa ya CAF kwaajili ya michuano hiyo
Ni wazi sasa Yanga haitasafiri nje ya Tanzania katika mechi zake za hatua ya awali zitakazopigwa August 16-18 na August 24-26
Yanga inatarajiwa kutumia uwanja wa Benjamin Mkapa katika mechi ya mkondo wa pili
Msimu huu Yanga imeweka malengo makubwa katika michuano ya ligi ya mabingwa ambapo Wananchi wanautaka ubingwa wa Afrika

No comments:

Post a Comment