Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, July 13, 2024

YANGA YATUMA SALAMU BURUNDI

 


Kile ambacho Yanga walikifanya kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika msimu uliopita walipokwenda Rwanda kucheza na Al Merrikh wamepanga kurudia tena watakapokwenda Burundi kumenyana na Vital'o katika hatua ya awali ya michuano hiyo msimu huu

Yanga itachuana na Vital'o August 17-18 nchini Burundi na mechi ya marudiano kupigwa wiki moja baadae Dar es Salaam
Meneja wa habari na mawasiliano Ali Kamwe amesema watafanya kampeni kubwa kuhakikisha Mashabiki wanakwenda kwa wingi Burundi kama walivyofanya msimu uliopita walivyokwenda rwanda
'Droo tumeiona na tumefurahi sana kwani tutahakikisha tunakwenda kuweka rekodi Burundi kama tulivyofanya Rwanda kucheza na Al Merrikh"
"Maandalizi yetu yanaendelea vyema Avic Town, huu ni msimu mwingine ambao tumeweka malengo ya kufanya vizuri zaidi. Ni mechi za mtoano ambazo hupaswi kumdharau mpinzani wako"
"Akili yetu sasa inaziwaza dakika 180 hizi dhidi ya Vital'o tukishamaliza ndio tutaanza kuangalia mchezo unaofuata utakuwaje," alisema Kamwe
Kama Yanga utavuka hatua ya awali raundi ya kwanza itachuana na mshindi wa mchezo kati ya SC Villa ya Uganda naCommercial Sports ya Ethiopia

No comments:

Post a Comment