Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, July 21, 2024

RASTA WA HANS POPPE AFURAHIA KUTUA MSIMBAZI

 

 Na Mwandishi Wetu.

“Nimejisikia furaha kwa sababu nimekuja katika timbu ambayo nilikuwa naiota, nimekuwa naiwaza siku zote kwa hiyo nimefurahi kukutana na wenzangu. Wenzangu wamenipokea vizuri na nimejiandaa kwaajili ya kuipambania timu yangu”

 

Ni maneno ya mchezaji 'kiungo fundi wa mpira' Awesu Ally Awesu akiwa mazoezini kwa mara ya kwanza na kikosi cha wekundu wa msimbazi baada ya kutua nchini Misri.

 

Hatiamaye ametimiza ndoto ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Miamba wa Soka Nchini na Afrika Simba SC marehemu Zacharia Hans Poppe ya kumuona akikipiga kunako wekundu wa Msimbazi, Simba Sc.

 

Ni jicho la ziada la kutambua  vipaji la Hans Pope ndilo lililomuibua kwa mara ya kwanza Awesu Awesu. Aliwahi kuitwa Rasta wa Hans Poppe kutokana na utambulisho wake mkubwa wa mtindo wa nywele.

 

Ilikuwa kwenye nusu fainali ya FA kati ya Madini SC  dhidi ya Simba SC katika dimba la Sheikh Amri Abeid wa jijini Arusha uliopigwa mwaka 2017. Awesu Awesu akichezea Madini ya Arusha katika pambano lile alikiwasha na kuisumbua sana safu ya kiungo ya Simba.

 

Ndipo jicho la Zacharia Hans Poppe lilipomuona kijana mwenye Rasta ambaye aliisumbua  kweli kweli Simba. Katika pambano hilo Simba walishinda kwa taabu 1-0.

 

Baada ya pambano lile Hans Poppe alipiga picha ya ukumbusho na Uwesu Awesu na kuzungumza naye mambo machache na inawezekana kubwa kabisa ni hapo baadaye atue Msimbazi

 

Ni baada ya miaka nane sasa Awesu Awesu ametua Msimbazi na yupo kambini Misri akijiwinda kwa msimu ujao wa mashindano mbalimbalj ikiwemo Ligi kuu ya NBC.

 

Akiwa Misri Awesu Awesu amekaririwa akieleza furaha yake ya kutimia kwa ndoto yake ya kutua katika timu ya moyo wake.

No comments:

Post a Comment